STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 25, 2014

Ronaldo, Benzema waipeleka Madrid kileleni Spain

 Real Madrid vs. Granada: La Liga Live Score, Highlights, Report
MABAO mawili ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Mchezaji Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo na Karim Benzema yameiwezesha Real Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Grenada katika pambano la Ligi Kuu ya Hispania.
Madrid walikuwa uwanja wa nyumbani na kujikuta wakibanwa hadi mapumziko wakiwa 0-0 na wageni wao kabla ya kipindi cha pili Ronaldo kufungua pazia kwa bao la dakika ya 56 kabla ya Benzema kuongeza la pili dakika ya 74.
Kwa ushindi huo Madrid imefikisha jumla ya pointi 53 na kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiziengua timu za Barcelona na Atletico Madrid zenye pointi 51 kila moja.





No comments:

Post a Comment