STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 25, 2014

Kun Aguero apiga hat trick akiibeba City ktk FA Cup

Sergio Aguero
Kun Aguero akiokota mpira nyavuni baada ya kufunga leo hat trick kwenye FA Cup
MSHAMBULIAJI aliyerejea tena dimbani baada ya kuwa nje kutokana na majeraha, Sergio kun Aguero, ameendeleza moto wake wa kufumania nyavu baada ya kuifungia Manchester City mabao matatu (hat trick) wakati wakiiangamiza Watford kwenye mechi ya raundi ya nne ya Kombe la FA.
City waliokuwa nyumbani walitanguliwa kufungwa mabao mawili ya haraka kupitia kwa Forestieri dakika ya 21 na Deeney dakika ya 30 na kudumua hadi mapumziko wenyeji wakiwa nyuma katika uwanja wa Etihad.
Hata hivyo kipindi cha kilianza kwa City kupigana kiume kurejesha mabao moja baada ya jingine, Kun akifunga dakika ya 60 na Aleksander Kalarov kusawazisha dakika ya 79 na Kun kuongeza mengin mawili dakika ya 87 na 93.
katika mechi nyngine za michuano hiyo Arsenal ilipata ushindi mnono mapema jana kwa kuizabua Coventry City kwa mabao 4-0, huku Nottingham Forest ikilazimishwa suluhu na Preston North End, AFC Bournemouth ikiwa nyumbani ilinyukwa na Liverpool kwa mabao 2-0, Sunnderland ikaendeleza makali yake kwa kuilaza Kidderminster kwa bao 1-0, Southampton ikashinda nyumbani kwa mabao 2-0 dhidi ya Yeovil Town na Huddersfield Town ililala kwao bao 1-0 dhidi ya Charlton Athletic.
Mechi nyingine za raundi hizo zilizochezwa pia leo zilishuhudia Hull City ikishinda ugenini 2-0 dhidi ya Southend Utd na Swansea City nayo ikishinda ugenini 2-1 dhidi ya Birmingham City, Wigan Athletic ikiishinda nyumbani kwa mabao 2-1 dhidi ya Sheffield Wednesday.

No comments:

Post a Comment