STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 6, 2014

Ajali nyingine basi la AM Coach lagongana na lori Tabora


Ajali mbaya ya basi la kampuni ya AM Coach lenya namba T 763 AYN imetokea leo asubuhi mkoani Tabora baada ya basi hilo kugongana na lori mali ya kampuni ya soda ya Coca Cola lenye namba za usajili T 256 BPP

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Tabora ajali hiyo ilitokana lori hilo kutaka kulipita basi bila kuwa makini na kisha kwa ufinyu wa barabara hiyo ndipo ikatokea 'mzinga' huo.
Mmoja wa abiria aliyenusurika alinukuliwa akisema kuwa;

"Dereva wa lori kajaribu kutukwepa lakini ufinyu wa barabara, mbele kuna lori scania linakuja,kwa hiyo akajikuta kagonga kushoto kwake na kulia kwake ila lori la kushoto kwetu halikusimama

Dereva wetu akashindwa kurudi upande wa kushoto kwa sababu kulikuwa na lori ambalo alikuwa anataka kulipita, basi letu lilikuwa 'linaovertake'(linataka kupita), basi nia AM Coach na lori ni la Coca Cola"

Bado haijafahamika madhara makubwa ya ajali hiyo ila taarifa zinafuatiliwa.
Ajali hiyo imekuja siku chache baada ya watu saba kupoteza maisha yao katika ajali mbaya iliyotokea eneo la Chalinze mkoani Pwani ikihusisha magari mawili ikiwamo Coaster iliyokuwa imebeba abiria.
EDDY

No comments:

Post a Comment