STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 6, 2014

Ujerumani, England, Ureno zaua kirafiki Ulaya


article-2574068-1C10556200000578-473_634x396
Ujerumani wakishangilia goli lao dhidi ya Chile
Ronaldo akipambana na kuweka rekodi ya mabao dhidi ya Cameroon walioizabua 5-1

Messi alishindwa kuibeba Argentina dhidi ya Romania
Italia walitepeta kwa Hispania 1-0, Diego Costa akiichezea timu yake hiyo kwa mara ya kwanza

Sturridge akishangilia bao liliuloibeba England jana
UJERUMANI usiku wa jana imefanikiwa kuizabua Chile kwa kuwalaza bao 1-0, huku England nayo ikipata ushindi kama huo kwa Denmark, na Brazili ikiifanyizia Afrika Kusini kwa kuifunga kwao mabao 5-0.
Bao la Ujerumani katika mechi yake na Chile lilifungwa na Mario Gotze aliyeshirikiana vyema na Mesut Ozil.
Matokeo mengine ya michezo ya kirafiki ya kimataifa inayotambuliwa na FIFA iliyochezwa jana na alfajiri ya leo Hispania iliilaza Italia baop 1-0 na kudhihirisha haikuiotea kwenye Fainali za Ulaya walipoisasambua mabao 4-0 mpaka kumfanya Mario Balotelli kumwaga chozi.
Mexixo na Nigeria zenyewe zilishindwa kufungana, Ivory Coast ikitoka sare ya mabao 2-2  na Belgiaum, huku Ureno ikiifumua Cameroon kwa mabao 5-1 Cristiano Ronaldo akifunga mawili na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji wenye mabao mengi kwa timu ya taifa lake akimzidi Pauleta.
amabaoUshirikiano wa kiungo wa Bayern Munich Mario Gotze na kiungo wa Arsenal Mesut Ozil ulizaa matunda jana usiku katika mchezo wa kirafiki baina ya Ujerumani dhidi ya Chile.
Wachezaji wawili walishirikiana vizuri katika goli la ushindi lilofungwa na Gotze kutoka na pasi nzuri ya mwisho ya Ozil. Mchezo ulimalizika kwa matokeo ya 1-0.

Matokeo Mengine ni kama ifuatavyo
Japan     4 - 2     New Zealand    
Iran     1 - 2     Guinea    
Russia     2 - 0     Armenia    
Bulgaria     2 - 1     Belarus    
South Africa     0 - 5     Brazil    
Algeria     2 - 0     Slovenia    
Namibia 1-1 Tanzania
Greece     0 - 2     Korea Republic    
Hungary     1 - 2     Finland    
Montenegro     1 - 0     Ghana    
Czech Republic     2 - 2     Norway    
Israel     1 - 3     Slovakia    
Bosnia-Herzegovina     0 - 2     Egypt    
Cyprus     0 - 0     Northern Ireland    
Colombia     1 - 1     Tunisia    
Turkey     2 - 1     Sweden    
Romania     0 - 0     Argentina        
Ukraine     2 - 0     United States    
Austria     1 - 1     Uruguay    
Switzerland     2 - 2     Croatia    
Germany     1 - 0     Chile    
Republic of Ireland   1 - 2     Serbia    
Belgium     2 - 2     Côte d'Ivoire    
Poland     0 - 1     Scotland    
Wales     3 - 1     Iceland    
France     2 - 0     Netherlands    
England     1 - 0     Denmark    
Australia     3 - 4     Ecuador    
Portugal     5 - 1     Cameroon    
Spain     1 - 0     Italy    
Honduras     2 - 1     Venezuela    
Mexico     0 - 0     Nigeria        
Costa Rica     2 - 1     Paraguay

No comments:

Post a Comment