STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 20, 2014

kun Aguero awindwa Barca, Martino ataja wengine saba

Kun Aguero
MSHAMBULIAJI nyota wa Manchester City, Sergio 'kun' Aguero ni kati ya wachezaji wanaomezewa mate na kocha mkuu wa Barcelona, Tata Martino.

Kocha huyo amewasilisha majina ya wachezaji nane anaotaka kuwasaji katika majira ya joto kwa Mkurugenzi wa Michezo wa klabu hiyo, Andoni Zubizarre.
Anayeongoza katika orodha hiyo ni mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero, wakati mkongwe wa Lazio Miroslav Klose naye akiwamo
Winga wa Atletico Madrid, Arda Turan na wa Borussia Dortmund,  Ilkay Gundogan watakuwa ni viungo wawili kwa Martino, wakati Santiago Vergini (anayecheza kwa mkopo Sunderland), Filipe Luis (Atletico Madrid), Doria (Botafogo) na Neven Subotic (Borussia Dortmund) wakitarajiwa kuimarisha safu yake ya ulinzi.
Barceloina imepania kujiimarisha zaidi ili kuendeleza kutamba kwenye ligi ya nchini mwao na michuano ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment