STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 8, 2014

Anelka amfuata Ronadinho Brazil

Nicolas Anelka
MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa, Nicolas Anelka amejiunga na Atletico Mineiro na kuungana na nyota wa zamani wa klabu mbalimbali za Ulaya, Ronaldinho, kwa mujibu wa rais wa klabu hiyo ya Brazil, Alexandre Kalil.
Anelka (35) hana klabu tangu alipotimuliwa na West Brom mwezi uliopita baada ya kushangilia goli alilofunga katika sare ya 3-3 dhidi ya West Ham Desemba mwaka jana kwa staili ya saluti ya Hitler.
Chama cha soka England (FA) kilimfungia mechi tano na kumtoza faini ya paundi 80,000 kwa kosa hilo.

No comments:

Post a Comment