STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 8, 2014

TFF yazithibitisha zilizopanda Ligi Kuu 2014-2015

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/ndanda%20uwiiiiiiiiiiiii.jpg?itok=eDereNWK
Timu ya Ndanda FC iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiaJ14FtkVg1y8zrjK8LdjzREEGxgzh8IN3GKVznVp2K0mMuy8ZF2EeEY2Fgm5LWFXYO6O2VDZQeN1wUHd3SAl4fu0kdvqgHu-50NZqtOhZ4J9zg7f2-xJa8bAXhgn1m-g1DrMLkC7FZ7bl/s1600/KIKOSI+POLISI.jpg
Polisi Moro iliyorejea Ligi Kuu kwa mara nyingine tena
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limezithibitisha timu za Ndanda SC ya Mtwara, Polisi ya Morogoro na Stand United ya Shinyanga kupanda daraja kutoka la Kwanza, kwenda Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao.
Taarifa ya TFF leo, imesema timu tatu za Ligi Daraja la Kwanza zitacheza Ligi ya Mkoa katika mikoa yao msimu ujao baada ya kushika nafasi za mwisho katika makundi yao, hivyo kushuka daraja.
Transit Camp imeshika nafasi ya mwisho katika A wakati Mkamba Rangers imeshuka daraja kwa kukamata mkia katika kundi B. Nayo Pamba SC imerudi kucheza Ligi ya Mkoa wa Mwanza baada ya kuwa ya mwisho kwenye kundi C.
Timu zilizopanda daraja kutoka FDL kwenda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao ni Ndanda SC ya Mtwara kutoka kundi A, Polisi Morogoro ya kundi B na Stand United ya Shinyanga iliyoibuka kinara katika kundi C.

No comments:

Post a Comment