STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 9, 2014

Rais Kikwete awaongoza maelfu kumlilia Mzee Small

Rais Kikwete akishiriki kwenye dua ya kuuombea mwili wa Mzee Small nyumbani kwa marehemu
Rais wa TAFF, Simon Mwakifamba akiwa na Juma Mbizo
Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Nyerere akiwa na Mkwere Original

Wazee wa Mizengwe walikuwapo
Mbembe akilia huku akitulizwa na Mafumu BIlal 'Bombega'
Wazee walikuwa makini kuhakikisha hali ya usalama

Kitwana Manara akiwa na wadau wenzake wa sanaa kwenye msiba huo
Nyota wa filamu, Shamsa Ford, Deo Shija, Cathy na Sandra nao walikuwapo

Issa Kipemba naye alikuwapo
Mashaka aliyeipa kamera mgondo akiteta jambo na Steve Nyerere na MC, Mkwere Original

Ramsey akiteta jambo na Niva
Mama Abdul na waombolezaji wengine

Mzee JKengua na Mzee Jangala walikuwapo bega kwa bega kwenye msiba huo

Maskini mzee wetu tangulia 'ticha' sisi tu nyuma yako
Shamsa Ford na wenzake








Masheikh wakiendesha kisomo kumuombea Mzee Small katika safari yake ya Ahera

Mtoto wa Marehemu, Muhidini Said

JB akiwa na George Kayanda
JB akihojiwa na wanahabari
Pole sana kijana, Rais Kikwete akiteta na mtoto wa marehemu Mzee Small


Rais akisaini kitabu cha maombolezo
 



Rais Kikwete akiteta na Rais wa TAFF, Simon Mwakifamba

Mzee Jangala akihojhiwa

Richie naye akihojiwa na Saida Mwilima wa Star TV

Mwili ukiombewa dua baada ya kuswaliwa

Mwili ukiswaliwa swala ya Jeneza kabla ya kupelekwa kuzikwa

Mtoto wa marehemu akisoma wasifu wa marehemu

Wazee wa Ze Comedy Show nao walikuiwapo

Safari ya kwenda kuzikwa inanza

Add caption




RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete leo amewaongoza maelfu ya waombolezaji waliojitokeza kumsindikiza kwenye makazi ya milele aliyekuwa mchekeshaji maarufu na mkongwe nchini, Said Ngamba 'Mzee Small'.
Rais Kikwete aliwaongoza waombolezaji hao waliojitokeza nyumbani kwa marehemu Mzee Small, Tabata Kisiwani jijini Dar es Salaam wakiwamo wasanii mbalimbali nyota na wanamuziki majira ya mchana wakati wa kisomo cha kumrehemu marehemu kabla mwili wake haujaenda kuzikwa jioni.
Rais Kikwete alipokewa kwenye msiba huo na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba na Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steven Nyerere na kupitiliza moja kwa moja hadi ndani kwenda kumpa pole mjane wa marehemu.
Baada ya robo saa alitoka na kwenda kuungana na waombolezaji wengine kwa kutia saini kitabu cha rambirambi kabla ya kuteta na mtoto wa marehemu Muhidini Said na kumkabidhi bahasha yenye risala yake na kisha kuondoka msibani hapo.
Mbali na Rais Kikwete, Rais wa TAFF na Mwenyekiti wa Bongo Movie, msiba huo ulihudhuriwa na nyota mbalimbali wa fani ya sanaa wakiwamo wacheza filamu kama JB, Richie, Dk Cheni, Shamsa Ford, Deoi Shija, Niva, Nova, Slim Omar, Mzee Chillo, Mzee Jangala, Sandra na wengine.
Miongoni mwa wanamuziki waliokuwepo kwenye msiba huo ni pamoja na Roman Mng'ande 'Romario' wa Msondo Ngoma, Cosmas Chidumule, Mafumu Bilal 'Bombenga' na waigizaji waliowahi kufanya kazi na marehemu enzi za uhai wake pamoja na Rais wa SHIWATA, Cassim Twalib 'Teacher'.
Baadhi ya wasanii akiwemo Steve Nyerere na Mzee Jangala waliuelezea msiba huo kuwa ni pigo kubwa siyo kwa familia ya marehemu bali wasanii wote kutokana na ukweli Mzee Small alikuwa mmoja wa waasisi wa michezo ya kwenye runinga na mkongwe aliyewasaidia vijana wengi akiwa kama mwalimu.
Pia walisema kifo cha Mzee Small umekuja kuwatonesha donda ambalo bado halijapona la kuondokewa na wasanii mfululizo ndani ya muda wa mwezi mmoja sasa.
HISTORIA YAKE KWA UFUPI
Marehemu Mzee Small alizaliwa mwaka 1955. Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Mingumbi, Kilwa mkoani Lindi. 

Mbali na ukongwe, Mzee Small kila alipozungumza na watu hakuona sababu ya kuficha kusema yeye ndiye msanii wa kwanza kabisa Tanzania Bara kuchekesha runingani.?
Mzee Small alianza sanaa hiyo miaka ya sabini akifundishwa na mwigizaji Said Seif ‘Unono’ ambaye ni marehemu kwa sasa.
Mbali na kushiriki sanaa katika vikundi mbalimbali, Mzee Small ametumika katika vikundi vya mashirika mbalimbali nchini.
Marehemu kila alipotajiwa Bi. Chau alisema ni mkewe wa ndoa wa kwenye maigizo kauli ambayo wengi hawakuiamini wakijua anakwepa kumtambulisha moja kwa moja.
Kuna wakati mke wake, Fatuma Ngamba aliwahi kusema kwamba, hana wivu na Bi. Chau kwa vile anajua anaigiza na marehemu na ndiyo kazi inayowafanya waishi.
Katika kipindi cha mateso ya ugonjwa wake, wadau mbalimbali walijitokeza kumsaidia kwa hali na mali huku wito mkubwa ukitolewa kwamba, watu zaidi wajitokeze badala ya kusubiri kutoa rambirambi.
Mzee Stori alianza kuigiza mwaka 1980 na kupitia makundi kadha kabla ya kuanzisha lake liitwalo Afro Dance.

Ameacha mjane na watoto sita pamoja na wajukuu saba.
Mwenyezi Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu Mzee Small. Amina.

No comments:

Post a Comment