STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 24, 2014

KIVUMBI AFRIKA AS VITA vs TP MAZEMBE NI SHIIIDA!

http://ptblog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2014/04/mazembe.jpg
TP Mazembe
https://lh5.googleusercontent.com/-WVEVQ9rwWPA/T4sgtVuUV_I/AAAAAAAASJ0/i37zP2UN0W0/IMG_0282.jpg?imgmax=800
AS VITA
KIVUMBI za mechi za kuhitimisha hatua ya makudni kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika kinatarajiwa kutimka vumbi leo kwa klabu nane zitakazposhuka dimbani kumalizia viporo vyao kabla ya kuruhusu kuanza kwa mechi za nusu fainali za michuano hiyo mikubwa.
Vita Club itakuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani kupepetana na 'ndugu' zao TP Mazembe kuwania uongozi wa kundi A wa Ligi ya Mabingwa Afrika, huku timu za Esperance ya Tunisia ikiialika Al Ahly Benghazi wa Libya mjini Tunis katika mechi nyingine kamambe.
Katika michuano ya Kombe la Shirikisho AC Leopard ya Congo itaialika ASEC Memosa ya Ivory Coast, huku Real Bamako ya Mali itaialika Coton Sports ya Cameroon katika pambano jingine la kukata na mundu la michuano hiyo.
Pambano la la mahasimu DR Congo As Vita dhidi ya Mazembe ndizo zinazosubiriwa kwa hamu na amshabiki kutokana na upinzani wao na wengi kutaka kuona kama Vita italipa kisasi kw akipigo ilichopewa na TP Mazembe katika mechi yao ya mkondo wa kwanza.
Pia Vita imekuwa nyonge kwa wapinzani wao hata kwenye Ligi Kuu ya DR Congo, hivyo mechi yao leo licha ya kutaka ushindi ili kujihakikishia nafasi ya kwanza ya kundi hilo, lakini pia kulinda heshima yao dhidi ya mahasimu wao wanaotamba na nyota wa Tanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.

No comments:

Post a Comment