STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 28, 2014

Michel Platin achomoa kuwania Urais FIFA

KATIKA kinachoonekana kama kumgwaya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter, Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya,UEFA, Michel Platini amesema hatagomea nafasi hiyo ya dunia kama ilivyokuwa ikivumishwa.
Platin amesea ni vyema kutilia mkazo kibarua chake cha sasa kuliko UEFA badala ya kushiriki uchaguzi huo wa FIFA.
http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2011/5/31/1306848649705/Michel-Platini-and-Sepp-B-007.jpg
Platin (kushoto) na Blatter
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa alikuwa akiaminika kuwa anafikiria kugombea nafasi nhiyo lakini alifafanua katika mkutano wa vyama 54 vya soka barani Ulaya uliofanyika huko Monte Carlo kuwa atabakia katika nafasi yake hiyo.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA, Michel D’Hooge alikaririwa akidai kuwa ni ujumbe chanya uliotolewa na Platini na amefurahi kwani inamaanisha kuwa safari hii hakutakuwa na ushindani kati FIFA na UEFA. 
Platini amekuwa akimkosoa vikali Blatter kwa zaidi ya mara moja na mapema mwaka huu alieleza kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 78 amekwisha kama mtu sahihi wa kuiongoza FIFA. 
Blatter aliwahi kudai kuwa ataachia ngazi mwishoni mwa muhula wake huu wa nne lakini alibadili mawazo na uamuzi wake baadae na kuweka wazi kuwa atatetea tena kiti chake katika uchaguzi ujao. 
Blatter amekuwa akifanya kazi FIFA toka mwaka 1975 na alichaguliwa kwa mara ya kwanza kushika nafasi ya urais mwaka 1998.

No comments:

Post a Comment