STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 28, 2014

Misri yaongeza idadi inayowania AFCON 2017

CHAMA cha Soka nchini Misri kiomeongeza idadi ya nchi zinazowania uaandaaji wa Fainali za Afrika 2017 baada ya kujitosa kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho Tanzania nacho imeingia tangu juzi.
Misiri ilianda mara ya mwisho fainali hizo mwaka 2006 na inawania nafasi hiyo na nchi nyingine baada ya waliokuwa wawe wenyeji, Libya kutangaza kujitoa.
Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Libya viwalazimisha kujitoa kwa mara ya pili baada ya mwaka jana kushindwa na kuiachia Afrika Kusini kuandaa.
Kutokana na hali hiyo ambayo imeikwaza nchi hiyo kutekeleza mikakati ya ujenzi wa viwanja na kuifanya Shirikisho la Soka Barani Afrika-CAF kutafuta mwenyeji mwingine wa michuano hiyo. 
Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya EFA kimebainisha nia ya kutaka kuwa mwenyeji wa michuano hiyo lakini bado hawajafanya uamuzi wa mwisho kuhusiana na suala hilo. 
Makamu wa rais wa EFA Hassan Farid naye alithibitisha nia yao hiyo lakini amesema bado wanataka kuzungumza na baadhi ya wizara serikalini ili kupata ushirikiano wao. 
Misri ni mojawpao ya nchi chake barani Afrika zenye miundo mbinu mizuri ya kuandaa michuano mikubwa kama Afcon.

No comments:

Post a Comment