STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 28, 2014

Kavumbagu hashikiki, Ruvu Shooting 'kavukavu'


http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/09/DSC04592.jpg
Kavumbagu (kushoto) akishangilia moja ya mabao yake na wachezaji wenzake wa Azam
WAKATI Didier Kavumbagu akiendelea kuongoza kwenye orodha ya wafungaji wa mabao mpaka sasa ligi ikiwa imemaliza mechi za raundi ya pili, Ruvu Shooting inayonolewa na kocha Tom Oloba ndiyo timu pekee ambayo haijaambulia pointi hata moja mpaka sasa.
Pia Ruvu ni kati ya timu mbili ambazo hazijatikisa wavu wa timu pinzania katika ligi hiyo ikienda sambamba na ndigu zao wa JKT Ruvu ambayo leo imefumuliwa mabao 2-0 na Kagera Sugar jijini Dar es Salaam.
Azam wamekalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo licha ya kulingana kila kitu na Mtibwa Sugar kutokana na kubebwa na herufi A.
Ndanda waliokuwa wakiongoza msimamo huo baada ya mechi za ufunguzi, imeporomoka hadi katika nafasi ya nne ikipitwa na Mbeya City wanaokamata nafasi ya tatu.
Didier ndiye kinara wa mabao mpaka sasa akiwa na mabao manne, hali inayoashiria kwamba Yanga walifanya kosa kubwa kumuacha mchezaji huyo kutoka Burundi aondoke Jangwani ilihali kwa misimu miwili mfululizo akiwa na kikosi hicho alikuwa kinara wa mabao ya Yanga.
Hata hivyo ni mapema kutabiri kama Kavumbagu atatimiza ndoto za kutwaa kiatu cha Dhahabu alichokikiosa kizembe msimu wa 2012-2013 baada ya kuzidiwa na Kipre Tchetche licha ya kumaliza duru la kwanza la msimu huo akiongoza orodha ya wafungaji.
Didier anafuatiwa na Ame Ally na Shomary Ally wa Mtibwa wenye mabao mawili kila moja huku orodha ya wachezaji wenye bao moja moja ikiongozwa na nyota wa Simba na Yanga, Emmanuel Okwi na Coutinho walianza kufunga mabao katika mechi zao za wikiendi hii dhidi ya timu za Polisi Moro na Prisons.


MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                                P  W  D  L  F  A  Pts
1. Azam                                   2   2   0   0  5   1   6
2. Mtibwa Sugar                     2   2   0   0  5   1   6
3. Mbeya City                        2   1   1    0  1   0   4
4. Ndanda Fc                          2   1    0   1  5   4   3
5. Prisons                                2   1    0   1  3   2   3
6.Kagera Sugar                      2    1   0   1  2   1   3
7.Yanga                                   2    1    0  1  2   2   3
8. Mgambo JKT                     2    1   0   1  1    1  3
9.Stand Utd                             2    1   0   1   2   4  3
10.Simba                                 2    0   2   0   3   3  2
11.Coastal Union                    2    0   1   1   2   3  1
12. Polisi Moro                       2    0   1    1  2   4  1
13.JKT Ruvu                          2    0   1    1  0   2  1
14. Ruvu Shooting                  2    0   0    2  0   4  0

No comments:

Post a Comment