STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 6, 2014

Man City Majanga, Chelsea yabanwa Ulaya, Bayern haoooo!

Eden Hazard missed the chance to win the match for Chelsea against Maribor late on when his penalty was saved
Hazard akipiga penati iliyookolewa wakati Chelsea wakitoka sare ya 1-1
Seydou Doumbia heads CSKA Moscow into an early lead as he takes advantage of a static Manchester City defence
Man City wakiadhibiwa na Doumbia
Toure jumps for joy as he celebrates levelling the score in what was a crunch match for City in the Champions League
Yaya Toure akishangilia bao lake jana
City's miserable night, and their campaign, was summed up by Toure's red card as he followed Fernandinho to the dressing room
Kisha akaja akalimwa kadi nyekundu ya kwamba maisha yake Etihad
Gotze is mobbed by his Bayern team-mates after doubling the Germans' lead late in the second half
Wachezaji wa Bayern Munich wakishangilia mabao yao yaliyowapeleka kwenye 16 Bora ya Ulaya
Ribery celebrates opening the scoring after Bayern had dominated possession in the first half
Fracky Ribery akishangilia bao la kwanza la Bavarians
WAKATI mabingwa watetezi wa England Manchester City wakigaragazwa nyumbani na kujiweka katika nafasi finyu ya kufuzu hatua ya 16 Bora ya Ligi ya mabingwa, Chelsea wameponea chupuchupu baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Maribor walioitandika vibaya wiki iliyopita.
Cheslea katika mechi ya Kungi G ilishtukizwa kwa bao lililofungwa dakika chache baada ya kipindi cha pili kuanza baada ya Agim Ibraimi kuifungia Maribor, kabla ya Nemanja Matic kusawazisha katika dakika ya 73.
Wakiwa na nafasi ya kuendeleza rekodi ya kipigo cha Maribor, Chelsea walipoteza penati baada ya mshambuliaji Eden Hazard kushindwa kukwamisha mpira wavuni.
Hata hivyo matokoe hayo bado yameiacha Chelsea kileleni mwa msimamo wa kundi hilo wakiwa na pointi nane wakifuatiwa na Schalke 04 iliyolala ugenini kwa mabao 4-2 mbele ya Sporting yenye pointi tano.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, Manchester City walijikuta wakijiweka pabaya kwa kukubali kipigo cha mabao 2-1 nyumbani dhidi ya CSKA Moscow, huku ikiwapoteza nyota wake wawili, akiwamo Yaya Toure aliyefunga bao pekee la timu hiyo.
Yaya alilimwa kadi ya pili ya njano na kusindikizwa na nyekundu na kuwa kadi yake ya kwanza tangu aanze kuichezea timu hiyo na tayari amewaomba radhi mashabiki wa klabu hioyo ya Etihad.
CSKA Moscow waliwashtukiza wenyeji kwa bao la mapema la dakika ya pili kupitia Seydou Doumbia akimalizia kati ya Natcho kabla ya Yaya Toure kusawazisha dakika sita baadaye ma Doumbia akamaliza udhia dakika ya 34 kwa kufunga bao la pili na katika kipindi cha pili wenyeji kuwapoteza Yaya na Fernandinho.
Kipigo hicho kimeiacha City wakiwa wanaburuza mkia wakiwa na pointi mbili wakitakiwa kupata ushindi mfululizo dhidi ya  Bayern Munich waliofuzu baada ya kuilaza Roma kwa mabao 2-0 na ile dhidi ya Roma wenyewe ambao wanashika nafasi ya pili wakilingana pointi na CSKA.
Katika mechi nyingine Porto ya Ureno ikiwa ugenini nchini Hispania ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Athletico Bilbao, huku Shakhtar Donetsk ya Uturuki wakiichakaza BATE kwa mabao 5-0 katika mechi za kundi H.

No comments:

Post a Comment