STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 6, 2014

Simanzi! Ajali yachinja watu 12 Ifakara

http://rantsofasassystew.com/wp-content/uploads/2011/10/Breaking_News.jpg
HABARI zilizotufiki hivi punde zinasema kuwa kumetokea ajali mbaya iliyohusisha basi la Al Jabir ambalo lililigonga Treni na kusababisha vifo vya watu 12 papo hapo wakiwamo watoto wawili.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Morogoro ni kwamba ajali hiyo ilitokea majira ya saa 9 katika eneo la Kiberege, Ifaraka wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.
Taarifa hizo zinasema kuwa basi hilo lenye namba za usajili T 725 ATD liliigonga Treni ya TAZARA na kusababisha roho za wanaume sita, wanawake wanne na watoto wawili waliokuwa kwenye basi hilo kupotea huku abiria wengine kuachwa na majeraha ya kutisha.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul amethibitisha taarifa hiyo na uchunguzi dhidi ya ajali hiyo unaendelea kujua chanzo chake.

No comments:

Post a Comment