STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 6, 2014

Wape Salam kuzinduliwa J2, Jahazi, King Majuto kunogesha

Kava la filamu ya Wape Salam
Bango la onyesho hilo la Jumapili
Ujio mpya wa Ulimwengu wa Filamu ndanio ya TBC1, Kibirigi a.k.a Kisate ndani

KUNDI la muziki wa taarab la Jahazi Modern linatarajiwa kupamba uzinduzi wa filamu mpya iitwayo 'Wape Salamu Zao' utakaoenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya pili ya kipindi cha Ulimwengu wa Filamu cha kituo cha TBC1.
Kwa mujibu wa mmoja wa waratibu na mshiriki wa filamu hiyo, Jackson Kibirigi 'Kisate' uzinduzi huo utafanyika kwenye ukumbi wa Travertine Magomeni na Jahazi wataangusha burudani kusindikiza tukio hilo.
Kisate alisema amepanga kufanya uzinduzi wa aina yake ambao haujawahi kufanywa katika uzinduzi wowote wa filamu nchini.
“Nimepanga kuacha historia katika uzinduzi wa filamu ya 'Wape Salamu Zao'. Kuna vitu vingi ambavyo sijawahi kuwaonyesha watazamaji kupiotia kazi zangu za nyuma hivyo mashabiki watarajie makubwa Jumapili," alisema Kisate.
Kisate alisema uzinduzi huo utasindikizwa na Jahazi chini ya Mzee Yusuf ambaye ameahidi pia kutoa burudani ya aina yake pamoja na King Majuto na wasanii mbalimbali wa Bongo Movie na watu wengine maarufu watapata fursa ya kupiga picha kwenye zulia jekundu.
Muigizaji huyo alisema kwa ndani ya filamu hiyo wamecheza Fatuma Makongoro, Jackson Kibirigi, Dennis David, Khadija Jarufu na wengine ambao waliitendea haki.

No comments:

Post a Comment