STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 26, 2014

Mcheza Kriketi mahututi baada ya kupigwa na gongo uwanjani

MCHEZA Kriketi nyota wa nchini Australia, Phil Hughes yupo mahututi akiipania roho yake hospitalini mjini Sydney baada ya kugongwa kichwani na gongo la kuchezea mchezo huo wakati wa mechi ya Sheffield Shield.
Nyota huyo aliyeichezea mechi yake mechi 26 Australia ikiwemo michuano mitatu ya Ashes, amefanyiwa upasuaji na yupo kwenye kitengo cha wagonjwa walio katika uangalizi maalum.
Hughes, 25, aliyeichezea Australia Kusini dhidi ya Wales Kusini mpya katika michuano ya Sydney Cricket Ground (SCG), alipigwa na gongo hilo akiwa na helmet kichwani na Sean Abbott kabla ya kupoteza fahamu na kukimbizwa hospitali.
Mara baada ya tukio hilo mchezaji huyo alizimia uwanjani na kuwafanya madaktari kuharaakisha kumwahisha hospitalini alipofanyiwa upasuaji huyo, lakini inaelezwa hali yake bado tete na mamia wa mashabiki wake wakiendelea kumuombea apate nafuu haraka.

No comments:

Post a Comment