STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 26, 2014

Kipusa cha Kaole Kwanza kuanza kurushwa Jan 4

Mwenyekiti wa kundi la Kaole Kwanza, Thea
KUNDI la Kaole Kwanza linaloundwa na wasanii wa zamani wa Kaole Sanaa linatarajiwa kuanza kurusha tamthilia yao mpya iitwayo 'Kipusa' Januari 4, mwakani.
Mwenyekiti wa kundi hilo, Misayo Ndimbagwe 'Thea' aliliambia MICHARAZO mapema leo kuwa, tayari wameshakamilisha kila kitu juu ya kuanza kurushwa kwa igizo hilo ambalo limewashirikisha wasanii mbalimbali nyota nchini akiwamo Bi Hindu, Muhogo Mchungu, Davina, Kipemba, Nyamayao, Bi Staa, Bi Terry, Swebe na wengine.
Thea alisema kituo kimojawapo nchini ndicho kilichopewa jukumu la kuanza kurushwa kwa igizo hilo ambalo lilizinduliwa mapema mwaka huu mbele ya wadau ambao walitoa maoni yao kwa ajili ya kuboreshwa.
"Tumekamilisha kila kitu na tamthilia yetu itaanza kurushwa mapema mwakani na kituo kimoja cha hapa nchini, hivyo mashabiki wajiandae kupata uhondo walioukosa kwa muda mrefu," alisema Thea.
Aidha, Thea alidokeza kuwa baada ya igizo hilo kuanza kurushwa hewani wataanza mchakato wa kuzalisha filamu zao ambazo zitaanza kuingia sokoni kuanzia Februari.
"Tumepania kuwapa uhondo mashabiki wa fani ya uigizaji, baada ya igizo kuanza kurushwa tutaanza kazi ya kurekodi filamu zetu ambazo zitakuwa sokoni kuanzia Februari," alisema Thea, mmoja wa nyota wa filamu aliyepata jina kubwa kupitia Kundi la Kaole Sanaa

No comments:

Post a Comment