STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 26, 2014

Mizengo Pinda kuzindua albamu ya Family Singers Dec 7

Mkurugenzi wa kikundi cha uimbaji wa muziki wa Injili cha Family Singers, Daniel Masheto Jr akizungumza na wanahabari leo juu ya uzinduzi wa albamu yao utakaofanyika Desemba 7
Mwenyekiti wa Family Singers, Jonas Danny akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani) wakati akitangaza uzinduzi wa albamu yao uya pili ya 'Usilie' utakaofanyika Des 7 katika ukumbi wa PTA.
Bango lenyewe na uzinduzi huo
Kikundi chetu hatuimbi tu muziki wa Injili pia tunajitolea kuihudumia jamii. Mkurugenzi Masheto Jr akitoa ufafanuzi
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa albamu ya 'Usilie' ya kundi la waimbaji wa muziki wa injili la Family Singers.
Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Desemba 7, mwaka huu kwenye Ukumbi wa PTA maarufu kama Sabasaba, Temeke jijini Dar es Salaam na kusindikizwa na waimbaji wa muziki wa Injili na kwaya mbalimbali na wasanii wa Bongo Movie.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa kundi hilo, Daniel Misheto Jr, alisema hiyo ni albamu yao ya pili baada ya awali kutamba na ile ya 'Machozi Yatafutwa' na kwamba waziri mkuu ndiye atakayekuwa mgeni rasmi baada ya kuwasiliana naye na kuwathibitishia atakuwapo siku ya uzinduzi huo.
Misheto alisema kundi lao mbali na kushughulika na masuala ya uimbaji wa muziki wa Injili, pia limekuwa likijitolea kwa jamii kwa kutoa huduma mbalimbali ikiwamo ya afya na kwamba hata siku ya uzinduzi huo kutakuwa na huduma ya afya bure kwa wananchi kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana kabla ya kupisha huduma ya uimbaji itakayoongozwa na wasanii mbalimbali.
"Tunatarajia kuzindua albamu yetu ya pili iitwayo 'Usilie' na shughuli hiyo itafanyika Desemba 7 katika Ukumbi wa PTA na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ndiye atakayekuwa mgeni rasmi na viongozi mbalimbali wamealikwa na tutasindikizwa na wasanii kadhaa akiwamo Leah Mudy, AIC (T) Vijana Chang'ombe, Martha Mwaipaja na wengine kutoka nje ya nchi," alisema.
Naye Mwenyekiti wa Family Singer Jonas Danny, aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi siku hiyo kwa ajili ya kupata huduma ya afya itakayoendeshwa na madaktari 20 kutoka hospitali za Muhimbili,  Dk Kairuki na IMTU.

No comments:

Post a Comment