STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 26, 2014

Sepp Blatter azidi kuandamwa FIFA

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/01781/balt_1781366b.jpgRAIS wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter ameendelea kuandamwa baada ya Rais wa  Ligi ya Soka ya Ujerumani-DFL, Reinhard Rauball kumtaka rais huyo kujiuzulu nafasi yake.
Rauball alikaririwa na gazeti la Kicker akidai kuwa anadhani wakati wa Blatter kuachia nafasi hiyo umefika kutokana na kashfa mbalimbali ambazo zimeendelea kuliandama shirikisho hilo.
Kashfa ambayo inaiandama shirikisho hilo kwa sasa ni kuhusu ripoti ya uchunguzi ya Michael Garcia yenye kurasa 430 ambayo FIFA imegoma kuichapisha kwa kuogopa kukiuka sheria.
Rauball amesistiza kuwa kashfa hiyo inayohusu mchakato wa kutafuta wenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022 inapaswa kumpelekea Blatter kujiuzulu ili kulinda heshima ya michuano hiyo. Michuano hiyo imepangwa kufanyika Russia na Qatar.
Rauball alifafanua kuwa jambo hilo kabla ya kuzungumza na vyombo vya habari alimpigia simu Blatter na kumueleza mawazo yake kuhusiana na hilo

No comments:

Post a Comment