STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Man City yaiua Everton 1-0, yazidi kuipumulia Chelsea

Manchester City v Everton
Yaya Toure akitumbukiza penati yake wavuni kuibeba Manchester City dhidi ya Everton
BAO la mkwaju wa penati lililofungwa na Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure yameiwezesha Manchester City kupatya ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Everton na kupunguza pengo la pointi dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea kufikia pointi tatu tu.
Toure alifunga bao hilo katika dakika ya 24 baada ya Phil Jagielka kumchezea rafu James Milner na yeye kutofanya ajizi kuukwamisha mpira kimiani na kuifanya City ambao ni mabingwa watetezi kufikisha pointi 33 na kung'ang'ania nafasi ya pili nyuma ya Chelsea ambayo mapema leo mchana ilikubali kipigio cha mabao 2-1 toka kwa wenyeji wao Newcastle United na kusitishiwa mfululizo wake wa ushindi katika msimu huu.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea siku ya Jumatatu kwa pambano moja tu litakaloikutanisha Southmapton dhidi ya Mashetani Wekundu, Manchester United.

No comments:

Post a Comment