STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Newcastle United yaiadabisha Chelsea, Cisse shujaa

Newcastle striker Papiss Cisse puts his side in front against Chelsea
Cisse akimtungua kipa wa Chelsea
Papiss Cisse scores for Newcastle against Chelsea
Cisse alikuwa na kazi ya kufunga tu St James Park
MABAO mawili ya mtokea benchi, Demba Cisse yameiwezesha Newcastle United kusitisha rekodi ya ushindi mfululizo wa Vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea baada ya timu hiyo kucharazwa mabao 2-1.
Cisse aliyeingizwa dimbani kipindi cha pili alidhihirisha umuhimu wake katika timu hiyo baada ya kufunga mabao hayo akiunganisha korsi pasi za Mousa Sissoko katika dakika za 57 na 78  kabla ya Didier Drogba kuipatia Chelsea bao kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu dakika ya 83.
Adabu hiyo ilitokana na Steven Taylor kucheza rafu iliyofanya aonyeshwe kadi ya pili ya njano na kuunganishiwa nyekundu dakika ya 81, hata hivyo pamoja na Chelsea kucharuka matokeo yalisalia kuwa 2-1.
Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Chelsea kwa msimu huu na kuendeleza unyonge wake kwa Newcastle kwa mechi ya tatu mfululizo kila wanapoifuata nyumbani kwao St James Park.
Kabla ya klipigo hicho Chelsea ilikuwa imcheza mechi 23 bila kupoteza na 14 zikiwa za ligi na kukatisha ndoto za mashabiki wa klabu hiyo wakiifikia rekodi ya Arsenal iliyocheza mechi 49 katika msimu wa 2003-2005.

No comments:

Post a Comment