STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Atletico Madrid yaipumulia Real Madrid Hispania

Atletico Madrid's Jose Maria Gimenez (left) celebrates scoring the opening goalKLABU ya Atletico Madrid imewapumulia wapinzani wao wa jadi, Real Madrid baada ya jioni ya leo kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Elche.
Mabao ya Giménez dakika ya 16 na lingine la Mario Mandžukić dakika ya 53 yaliwapa ushindi mabingwa hao watetezi wa La Liga na kupunguza pengo lao la pointi dhidi ya Real Madrid na kuwa moja.
Atletico wamefikisha pointi 32 dhidi ya 33 za Real Madrid ambayo baadaye usiku huu itamenyana na Celta de Vigo.
Mbali na pambano la Real Madrid na Celta Vigo pia viwanja vingine vitawaka moto katika ligi hiyo ya Hispania.

No comments:

Post a Comment