STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Zlatan Ibrahimovic aipaisha PSG Ufaransa

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/70314000/jpg/_70314410_019566211-2.jpgMSHAMBULIAJI Zlatan Ibrahimovic amerejea dimbani kwa kishindo baada ya kuiongoza timu yake ya PSG kupata ushindi nyumbani wa mabao 2-1 dhidi ya Nates.
Ushindi huo umeifanya PSG kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Ufaransa.
Ibrahimovic aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu alifunga mabao hayo katika dakika ya 34  akimalizia kazi ya Lucas na katika dakika ya 48 kwa mkwaju wa adhabu ndogo na kuifanya watetezi hao wa Ligue 1 kufikisha pointi 37 kwa michezo 17 na kukaa kileleni.
Bao la wageni lilifungwa mapema katika dakika ya nane kupitia kwa Bedoya kabla ya wenyeji kucharuka na kulisawazisha na kuongeza la ushindi.

No comments:

Post a Comment