STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

Ruvu yanyakua mwingine, kukipiga na Friends Rangers kesho

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/11/MWOMBEKI.png
Betram Mwombeki aliyekuwa akiichezea Simba msimu uliopita ni mmoja ya walionyakuliwa na Ruvu Shooting
KLABU ya Ruvu Shooting ambaye kesho inatarajiwa kushuka uwanja wa Shule ya Mwalimu Nyerere (Makurumla) katika mechi ya kirafiki, imefanikiwa kusajili wachezaji wengine wawili akiwamo nyota wa zamani wa Chemlin na Sony Sugar, Mwita Semlonge John aliyetokea Toto Africans.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire alisema kuwa mchezaji huyo wa safu ya ushambuliaji ni wa tatu baada ya Betram Mwombeki na Yahya Tumbo.
Bwire aliongeza kuwa pia wamempandisha mchezaji mmoja toka timu ya vijana U20, Ally Yusuph kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao ambacho kesho kitawapima vifaa hivyo kwa kuumana na Friends Rangers katika pambano la kirafiki.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa kali kutokana na ukweli Friends imefanya usajili wa kuvutia katika dirisha dogo kwa kuwanyakua Haruna Moshi 'Boban', Amir Maftah na wengine kitu kinachofanya mtanange huo usio wa kitoto.

No comments:

Post a Comment