STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

Spurs yaitambia Swansea City kwao, yachupa EPL

Harry Kane clinches his first in celebration after putting Tottenham Hotspur 1-0 ahead against Swansea City at the Liberty Stadium
Harry Kane akifunga bao la lkuongoza la Spurs
Harry Kane
Eriksen akishangilia bao lililowapa Spurs ushindi wa 2-1 nyumbani kwa Swansea City
BAO la dakika za jioni lililofungwa na Christian Eriksen lilitosha kuwapa ushindi muhimu Tottenham Hotspur katika mfululizo wsa Ligi Kuu ya England.
Eriksen aliyehusika pia katika kutengeneza bao la kuongoza la Spurs lililowekwa kimiani kwa kichwa na Harry Kane katika dakika ya nne tu ya mchezo huo, alilifunga katika dakika ya 89 na kuifanya timu yake kuendeleza ubabe kwa Swansea City waliokuwa nyumbani kwao.
Pambano hilo lilionekana kama lingeisha kwa sare ya 1-1 baada ya wenyeji kufunga bao la kusawazisha dakika tatu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kupitia Winfried Bony.
Hata hivyo vijana wa Maurico Pochettino walicharuka na kusaka bao hilo muhimu lililofungwa na Eriksen na kuifanya Spurs kuchuopa hadi nafasi ya saba kwa kufikisha pointi 24 wakiporomosha Newcastle United ambayo jana ilinyukwa mabao 4-1 na Arsenal.
Ligi hiyo ya England inatarajiwa kuendelea kesho kwa mchezo mmoja tu kati ya Everton itakayoikaribisha QPR kwenye uwanja wa Goodson Park.

No comments:

Post a Comment