STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

Arsene Wenger awashukuru mashabiki

http://www.kooxaha.com/wp-content/uploads/2014/10/weng-kooxaha1.jpgKOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amewashukuru mashabiki waliokuwa wakiimba jina lake wakati timu hiyo iliporejesha makali yake ya ushindi katika Ligi Kuu.
Wenger, 65 alishambuliwa kwa kuzomewa na kutukanwa na mashabiki wa timu hiyo baada ya kipigo cha mabao 3-2 kutoka Stoke City wiki iliyopita.
Lakini katika mchezo dhidi ya Newcastle United uliochezwa jana na Arsenal walishinda mabao 4-1, mashabiki hao walisikika wakiimba nyimbo za kumsifu kocha huyo.
Akihojiwa na waandishi wa habar, Wenger amesema kazi yao ni kuhakikisha wanashinda mechi za soka na pindi wasipofanya hivyo huwa anawaelewa kwani hawafurahishwi.
Arsenal bado wako nyuma ya vinara Chelsea kwa alama 13 lakini ushindi wa jana ukichanganya na ule wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray kidogo umepandisha morali ya timu baada ya kipigo dhidi ya Stoke.
Pia huenda ikatuliza munkari ya mashabiki hao waliokerwa na kauli ya kocha huyo kwamba huenda asingefanya usajili wowote katika usajili wa mwezi Januari.

No comments:

Post a Comment