STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

Mashetani Wekundu waifumua Liverpool 3-0

Wayne Rooney, Man Utd
Rooney akifunga bao la kuongoza la Manchester United
Robin van Persie, Man Utd
Weweeeee! van Persie akishangalia bao lake na wachezaji wenzake
Mario Balotelli, Liverpool
Mario Balotelli akionyeshwa kadi ya njano, mshambuliaji huyo aliyekuwa majeruhi alichangamsha pambano hilo baada ya kuingia akitoka benchi, ingawa aliendelea kukosa mabao ya wazi mbele ya De Gea
JAHAZI la Liverpool limezidi kwenda mrama baada ya kutandikwa mabao 3-0 na Manchester United katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford, Mashetani Wekundu walianza kuiadhibu Liverpool iliyopo chini ya kocha Branden Rodgers katika dakika ya 12 wakati nahodha Wayne Rooney kuandika bao akimalizia kazi ya Valencia.
Dakika nne kabla ya mapumziko Manchester iliongeza bao la pili baada ya Juan Mata kumalizia kazi nzuri ya Robin van Persie.
Bao lililowanyong'onyesha 'vijogoo' vya Anfield, liliwekwa kimiani na van Persie akimalizia pasi murua kutoka kwa Juan Mata.na kuifanya Mashetani Wekundu kufikisha pointi 31 na kung'ang'ania nafasi ya tatu nyuma ya Chelsea inayoongoza kwa pointi 39 na Manchester City yenye pointi 36.
Hivi sasa dimbani Swansesa Cit inaumana na Tottenham Hotspur na wageni Spurs wako mbele kwa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment