STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 14, 2014

Simba yazidi kusajili wapya, Tambwe byebye!


seru
Simon Sserunkuma akisaini fomu za Simba
KLABU ya Simba imekatisha mkataba na wachezaji wake wawili wa kimataifa wote raia wa Burundi, ambao ni Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Tanzania, Mshambuliaji Amissi Tambwe na Kiungo Pierre Kwizera, siku moja tangu Simba kuifunga Yanga 2-0 katika pambano la Nani Mtani Jembe.
musheed
Mursheed akisaini mkataba wake leo
Simba, imevunja mkataba na wachezaji hao ili ipate nafasi ya kuwasajili nyota wa Kiganda, mshambuliaji Simon Sserunkuma na beki Juuko Murushid, ambao wamesanishwa mikataba yao leo.
Simon maarufu kama Sam Sserunkuma na Juuko Murushid, waliichezea Simba dhidi ya Yanga jana katika uwanja wa Taifa Jijini Dar-es-salaam, na wote walionesha uwezo mkubwa na kuisaidia Simba kupata ushindi huo wa mabao mawili dhidi ya Yanga.
Baada ya usajili huu sasa wachezaji wa kigeni kutoka Uganda wanafikia watano katika klabu hiyo, wakiongozwa na beki Joseph Owino, mshambuliaji Emanuel Okwi, Dan Sserunkuma, Simon Sserunkuma na Juuko Murushid.

Hata hivyo kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya usajili wa Simba, Zakaria HansPoppe kuwa Dan amepewa nafasi ya kupunguza kilo alizonazo.

No comments:

Post a Comment