STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 24, 2015

Breaking News: Waziri Prof Muhongo atangaza kujiuzulu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgofvT59YEKqnPi1tct_v_grVGvyKfclYGpMmBYSTtY0gNer1nQKkuaZLVla2I4kKMgccK2BxgsjRwv7R7ir3wuPloEP6HfBp4xKUDUmVr9KDZrWyiYZ23hkBw1IwEi1_jEW1woldsH3oz8/s1600/Prof.+Muhongo.jpg
Prof Muhongo aliyetangaza kuachia ngazi serikali asubuhi hii
HATIMAYE Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huo leo ikiwa ni karibu mwezi mmoja tangu kuwepo kwa shinikizo la kumtaka ajiuzulu nafasi hiyo kutokana na kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow.
Prof Muhongo ni miongoni mwa waliotajwa katika kashfa hiyo, lakini hakuchukuliwa hatua zozote na Rais Jakaya Kikwete wakati akilihutubia taifa, huku aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof Anna Tibaijuka akiondolewa kwenye nafasi yake kutokana na sakata hilo.
Maamuzi ya kuachia ngazi kwa Prof Muhongo yametolewa mbele ya wanahabari aliokutana nao asubuhi jijini Dar es Salaam.
Pamoja na kueleza mafanikio yake ndani na nje ya nchi kupitia wizara hiyo na kujitaja kama mtu msafi ambaye ana doa lolote, waziri huyo alitangaza kuachia ngazi kwa madai ya kutafakari kwa kina, ingawa kabla ya hapo alishawahi kunukuliwa kwamba asingejiuzulu ng'o.
Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kuwa hatua hiyo imekuja baada ya shinikizo kubwa kutoka kwa wakubwa wake, ikizangatiwa heshima aliyonayo kama Profesa.
Kujiuzulu kwake kumekuwa wakati Katibu wake, Eliakim Maswi kutimuliwa kazini na Katibu Mkuu Kiongozi kutokana na sakata hilo, huku watendaji kadhaa umma wakiburuzwa mahakamani wakikabiliwa na kesi zinazohusiana na sakata hilo la Tegeta Escrow.

No comments:

Post a Comment