STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 24, 2015

OCODE yawaokoa wanafunzi 651 kukaa chini Chanika

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tungini, Chanika wakiyajaribu mawadati waliokabidhiwa na OCODE
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tungini, wakiyakalia madawati waliyokabidhiwa
Wakiwa haamini kama hawatakaa tena chini baada ya shule yao kupewa madawati 100
Wazazi wa Shule ya Msingi Tungini walikuwa mashuhuda wa makabidhiano hayo
Wanafunzi walishangilia na kupongeza kwa makofi
Afisa Elimu Shule za Msingi, Ilala, Elizabeth Thomas alitoa nasaha zake katika hafla ya makabidhiano ya madawati 217 kwa shule tatu za manisapaa yake toka kwa OCODE
Mratibu Mkuu wa OCODE, Jackson Joseph akisoma risala kuelezea asasi yao na misaada wanayotoa kwa jamii ya Watanzania katika nyanja ya elimu na uchumi
Akaikabidhi risala hiyo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Rogasian Seda aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo aliyekuwa awe mgeni rasmi
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya OCODE, Vedasto Ngaiza naye akatoa nasaha zake kwa waalikwa
Mwenyekiti wa Bodi ya OCODE akakabidhi waraka wake kwa Mgeni Rasmi, Mchumi wa Manispaa ya Ilala aliye pia Kaimu Mkurugenzi, Rogasian Seda 
Kaimu Mkurugenzi wa Ilala, Rogasian Seda akimkabidhi cheti Mwalimu Mkuu wa Shule ya Tungini, Peter J Peter kuonyesha ishara ya kukabidhiwa msaada toka OCODE
Jamani madawati yenyewe ndiyo haya hapa kaimu Mkurugenzi wa Ilala (mwenye koti) na Afisa Elimu wakionyeshwa madawati na uongozi wa OCODE
Kaimu Mkurugenzi wa Ilala na Mwenyekiti wa Bodi ya OCODE wakishikana mkono kuonyesha ishara ya kukabidhiana madawati huku wakishuhudiwa na Mwalimu Mkuu wa Tungini, Peter J Peter (shati jeupe), Afisa Elimu (wa pili kushoto) na Mratibu wa OCODE, Jackson Joseph.
Wanafunzi wakayachangamkia kuyakalia kama ishara ya kuyapokea shuleni kwao
Mchumi wa Manispaa ya Ilala na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Rogasian Seda akitoa nasaha zake
Wanafunzi wakifuatilia kila tukio lililokuwa likiendelea katika hafla hiyo iliyofanyika Shule ya Msingi Tungini, Chanika jijini Dar es Salaam
Weweee hatukai tena chini ahsanteni OCODE, ahsanteni wazazi
Na Rahim Junior
WANAFUNZI zaidi ya 651 wa Shule za Msingi tatu za Tungini, Nzasa II na Msongola zilizopo Chanika, wilayani Ilala jiji la Dar es Salaam wameokolewa kukaa chini baada ya Asasi ya Maendeleo ya Jamii iitwayo Organization for Community Devlopment (OCODE) kuzikabidhi shule hizo msaada ya madawati 217 yenye thamani ya Sh. Milioni 21.
Aidha asasi hiyo imezisaidia kukarabati na kujenga majengo matatu ya madarasa yenye thamani ya Sh. Milioni 22 kwa Shule za Msingi Viwege na Msongola ambayo waliyakabidhi katika hafla zilizofanyika juzi na kushuhudiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, ambaye pia ni Mchumi wa Manispaa hiyo, Rogasian Seda aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa aliyekuwa awe mgeni rasmi wa hafla hiyo.
Msaada huo wa madawati na madarasa hayo ulikabidhiwa kwa wakuu wa Shule hizo juzi na kuhudhuria pia na Afisa Elimu wa Shule ya Msingi wilaya ya Ilala, Elizabeth Thomas ambaye aliushukuru uongozi wa OCODE kwa msaada huo na kutoa wito kwa asasi nyingine na wananchi kuendelea kujitolea kwa ajili ya maendeleo ya elimu nchini na kuwafanya watoto wafurahie kwenda shuleni kwa sababu ya mazingira mazuri.
Kabla ya makabidhiano hayo, Mratibu wa OCODE, Jackson Joseph alifafanua mgawanyo wa madawati hayo kwa kueleza kuwa, Shule ya Msingi Tungini yenyewe imepata madawati 100,  wakati Nzasa II ilipewa madaewati 72 na Msongola ilipewa madawati 45, ambayo kwa jumla yake itawafanya wanafunzi 651 kwa maana ya kila dawati moja wanakaa wanafunzi watatu kuokolewa kukaa chini kutokana na msaada huo.
"Kwa hapa Tungini tunakabidhi madawati 100, lakini tayari tumeshapeleka madawati 72 katika shule ya Nzasa II na 45 Msongola ambapo kwa idadi hiyo ya madawati 217 tutakuwa tumewaokoa wanafunzi 651 kuketi chini kama ilivyokuwa mwanzoni kwa kuwafanya sasa wakae katika madawati na kusoma kwa utulivu," alisema Jackson.
Aliongeza kuwa asasi yao ambayo iliasisiwa mwaka 1992 na kusajiliwa serikali mwaka 2003 ilikabidhi pia madarasa mawili kwa Shule ya Viwege, moja wakilikarabati na jingine likiwa kipya wakishirikiana na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo na jingine moja wamelikarabati katika Shule ya Msongola ambayo nao pia walikabidhiwa tayari kuwafanya wanafunzi wasome katika mazingira mazuri.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Rogasian Seda, licha ya kuishuruku na kuipongeza asasi ya OCODE pamoja na wazazi walioshiriki kuchangia michango mbalimbali ya shule zao, alisema bado manispaa hiyo ni tatizo sugu la madawati kwa shule zake.
Seda, alisema Ilala ina upungufu ya jumla ya madawati 12,000 na kwa bajeti ya mwaka huu wametenga kiasi cha madawati 2,100 tu hivyo kuwahimiza wazazi kuendelea kushirikiana na serikali na asasi za kijamii kama OCODE ili kupunguza tatizo hilo, huku akiwakumbusha wazazi na Kamati ya Shule za Ilala kulinda na kutunza vema misaada wanayopewa ili kuwaokoa watoto kukaa kwenye vumbi.
"Ni wajibu weenu kutunza misaada mnayopewa, wanafunzi tunzeni madawati yenu ili muendelee kuyakalia, msikubali yaharibike kwani mtataabika, kwa hakika Manispaa imefarijika kwa hili lililofanywa na OCOPDE na kuhimiza wengine kujitokeza," alisema Seda.
Kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Afisa Elimu wa Shule ya Msingi Manispaa ya Ilala, Elizabeth Thomas, alisema wamefurahishwa na juhudi ambazo zimekuwa zikifanyw ana OCODE na kuahidi kuwa nao bega kwa bega ili kuleta maendeleo ya elimu sawia na yale ya kiuchumi kwa wananchi wa manispaa hiyo.
Naye Mwenyekiti wa Bodi wa OCODE, Vedasto Ngaiza aliweka bayana kuwa asasi yao haitaondoka Ilala mpaka ihakikishe tatizo la madawati katika shule za Ilala linaisha kama walivyoweza kufanya Temeke kwa kuzisaidia Shule 24 ambayo waliweka kambi kwa zaidi ya miaka 10.
Ngaiza alisema kitu cha muhimu wazazi na kamati za shule kuhakikisha hawageuzi madawati wanaoyopewa kuwa kuni baada ya kuharibika bali wayatunze na kuyakarabati ili yaweze kuwasaidia watoto.
Pia alisema mikakati ya OCODE ambayo tangu Januari mwaka jana imeanza kutekeleza programu mbili za miaka mitano katika manispaa ya Ilala moja ikiwa ni kusaidia kwenye masuala ya Elimu na nyingine kuwainua wananchi kiuchumi kupitia miradi mbalimbali, lakini pia wanafikiria kusaidia kuzijengea shule za manispaa hizo uzio kwa ajili ya kuwafanya wanafunzi wasome sehemu salama wao na vifaa vyao kama madawati.
"Kwa hali kama hii tunayoiona shule ikiwa haina uzio, ni rahisi misaada kama hii kuibwa na madarasa kuanza kutumiwa kwa mikutano ya nguvu za giza, hivyo OCODE tunafikiria pia kusaidia kujengwa kwa uzio ili wanafunzi na mali za shule ziwe salama," alisema Ngaiza na kuamsha vigelegele toka kwa walimu wa shule hiyo na wazazi waliohudhuria sherehe hizo za makabidhiano Tungini.

No comments:

Post a Comment