STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 24, 2015

Prof Muhongo kujiuzulu uwaziri?

http://api.ning.com/files/17StHKe5zK7HSUrKU-HhrOv-dPDLCOp2bhaxh8P5xjEfQfYciwmCCausbIfHnM2VPo24wYqptCTGEAzK0unqbx4qNxHqFmZe/profmuhongo.JPG
Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo ambaye amekuwa akisakamwa kutokana na sakata za uchotwaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow anazungumza na wanahabari asubuhi hii.
Taarifa hizo hazijaweka bayana Prof Muhongo atazungumza kitu gani, lakini inadhaniwa huenda akatangaza kuachia ngazi katika nafasi hiyo kutokana na shinikizo kubwa lililopo ndani na nje ya serikali na chama chake cha CCM.
Hata hivyo kwa namna Waziri huyo alivyo ng'ang'ari inadaiwa huenda akatoa ufafanuzi juu ya tuhuma zinazoelekezwa kwake na kutakiwa kujiuzulu, japo Rais Jakaya Kikwete katika hutoba yake alisema amemweka kipioro Waziri huyo aliyetajwa kama 'Dalali' katika sakata zima la Escrow kwa mujibu wa ripoti ya PEC inayoongozwa na Mwenyeki wake, Zitto Kabwe.
MKICHARAZO itawaletea taarifa kamili juu ya mkutano huo unaofanyika jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment