STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Chelsea yakaribia kumnasa Cuadrado

http://resources2.news.com.au/images/2015/01/27/1227198/061530-6ca4ddec-a5bb-11e4-a11e-9d15a37a8504.jpg
Juan Cuadrado anayekaribia kutua Chelsea
VINARA wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Chelsea ipo katika hatua za mwisho kukamilisha dili la Pauni Mil. 23.3 ili  kumsajili winga wa Fiorentina Juan Cuadrado, 26.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia tayari ameshafikia makubaliano kuhusu mambo yake binafsi na Chelsea na kwa sasa klabu ziko katika hatua za mwisho kukamilisha uhamisho huo.
Inakadiriwa kuwa Chelsea watatoa kitita cha Pauni Mil.26.8 kwa ajili ya winga huyo kiasi ambacho ndio kilichowekwa na klabu yake hiyo ya Italia sambamba na kudaiwa kuwa mbioni kumtoa kwa mkopo kinda lake Mohamed Salah, 22 kwa klabu hiyo ya Fiorentina ikiwa ni sehemu ya kukamilisha dili hilo.
Hata hivyo, Salah ambaye ni winga wa kimataifa wa Misri bado hajaamua kama anataka kwenda kucheza Serie A au sehemu gani nyingine.
Aidha imedokezwa kuwawinga nyota wa Chelsea, Andre Schurrle yupo katika mazungumzo ya kutua klabu ya Bundesliga,Wolfsburg.

No comments:

Post a Comment