STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Diego Costa majanga! Afungiwa England

The Spain striker celebrates his goal in the 2-0 Premier League win over West Ham
Diego Costa aliyefungiwa mechi tatu kwa kosa la kumtimba Emre Can
STRIKA mkali wa klabu ya Chelsea, Diego Costa amefungiwa mechi tatu kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu kati ya timu yake na Manchester City utakaochezwa Stamford Bridge kesho pamoja na mechi dhidi ya Aston Villa na Everton. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kilimtwanga adhabu hiyo ambayo Costa aliipinga kuhusiana na tukio lake alilofanya katika dakika ya 12 ya mchezo wa nusu fainali ya mkondo ya pili wa Kombe la Ligi uliofanyika Jumanne iliyopita.
Costa aliyesajiliwa kwa kitita cha Pauni Mil. 32, ameshafunga mabao 17 katika mechi 19 za Ligi Kuu alizocheza simu huu.
Tukio hilo halikuonwa na waamuzi lakini lilinaswa katika picha za video na FA kutumia kama ushahidi wa kumtia adabu mshambuliaji huyo ambaye alikuwa akitetewa na kocha wake, Jose Mourinho.

No comments:

Post a Comment