STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Shamsa Ford amsifia Mama Muuza

MWANADADA nyota wa filamu nchini, Shamsa Ford amewataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea filamu yake moya iitwayo 'Mama Muuza'.
Shamsa aliyefanya vema mwaka uliopita kupitia filamu za 'Hukumu ya Ndoa Yangu' ya Jacob Stephen 'JB' na 'Chausiku' ambayo ni kazi binafsi alisema filamu hiyo mpya ipo jirani kutoka.
Muigizaji huyo alisema filamu hiyo ni miongoni mwa filamu anazotegemea kufanya vema mwaka 2015 kutokana na simulizi lake lilivyo na jinsi washiriki wake walivyoitendea haki.
Alisema ndani ya filamu hiyo imeshiriki wasanii wakali akiwamo yeye na Baba Haji.
"Mama Muuza ipo jirani kutoka, hivyo mashabiki wajiandae kuipokea kama walicvyoipokea Chausiku," alisema Shamsa Ford ambaye anatamba na kazi nyingine kadhaa zilizomweka katika orodha ya wasanii nyota nchini wa filamu.

No comments:

Post a Comment