STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Gerrard Pique, Shakira wapata mtoto wa pili

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/08/Shakira-Gerard-Pique-Milan.jpg
Shakira na Pique wakiwa na Milan
BEKI wa Barcelona, Gerard Pique na mwanamuziki nyota Shakira wamepata mtoto wao wa pili aliyezaliwa usiku wa jana.
Shakira alijifungua mtoto wa kiume bila matatizo yeyote katika hospitali ya Quiron Tecknon iliyopo jijini Barcelona.
Pique, 27 na mwanamuziki huyo wa Pop kutoka Colombia mwenye umri wa miaka 37, walitoa taarifa hizo muda mfupi kabla ya usiku wa manane.
Jina la mtoto ambaye amezaliwa miaka miwili baada ya wawili hao kupata mtoto wao wa kwanza aitwaye Milan Piqué Mebarak, ni Sasha Piqué Mebarak.
Wawili hao wamekuwa pamoja toka mwaka 2010 walipokutana katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment