STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Simba katika mtihani mwingine, kulipa kisasi kwa JKT kesho?

Simba watavuna nini kesho kwa JKT
JKT Ruvu kuendeleza machungu Msimbazi?
WAKATI Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola akiomba kuachia ngazi mwenyewe ndani ya klabu hiyo, timu hiyo kesho itakuwa na kibarua kingine kigumu mbele ya maafande wa JKT Ruvu katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Katika mechi ya mwisho baina ya timu hizo msimu uliopita, Simba ilicharazwa mabao 3-2 na maafande hao hali inayofanya mechi ya kesho miongoni mwa mechi zitakazochezwa katika viwanja tofauti kuwa ni kama vita ya kisasi.
Simba na JKT wataumana kwenye uwanja wa Taifa, huku timu hizo zikiwa na matokeo tofauti katika mechji zao zilizopita, Simba ikitoka kupokea kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City wakati JKT Ruvu wakilazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT.
Mechi nyingine zitakazopigwa kesho ni pamoja na zile za timu za Coastal Union dhidi ya Mtibwa Sugar mchezo utakaochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga, huku Prisons Mbeya itawalika Kagera Sugar uwanja wa Sokoine Mbeya na Polisi Moro waliotoka kucharazwa bao 1-0 na Yanga wataialika Mbeya City uwanja wa Jamhuri.
Mechi ya Mgambo JKT na Azam yenyewe imeahirishwa kwa kuwa Azam wapo DR Congo wakicheza mechi za kirafiki za michuano maalum.
Ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa michezo miwili Yanga itaikaribisha Ndanda ya Mtwara na Ruvu Shootimng itavaana na Stand United kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Mpaka sasa katika ligi hiyo Azam wapo kileleni wakiwa na pointi 21 wakifuatiwa na Yanga wenye pointi 18 sawa na JKT Ruvu.
Katika hatua nyingine uongozi wa Simba umesema umepata taarifa za Kocha Msaidizi wa timu yao Seleman Matola kutokana na kile kinachoelezwa kuwa kuitingwa na majukumu, japo inaelezwa kusakamwa na baadhi ya wanachama na viongozi wa klabu hiyo ni sababu ya Matola kuamua kubwaga manyanga.
Uongozi wa Simba kupitia Rais wake, Evance Aveva umesema kuwa umemtaka kocha huyo kuandika maombi yake kimaandishi ili kuyajadili na kutoa maamuzi, sambamba na kutoa sababu ya timu yao kuwa na matokeo mabaya katika mechi za karibuni kuwa inatokana na uchovu wa wachezaji kucheza mfululizo.
Wakati ligi ikiingia kwenye raundi ya 13 wikiendi hii chini ni msimamo na orodha ya wafungaji mpaka sasa.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam                 11  06  03  02  15  08  07   21
02. Yanga                10  05  03  02  12   07  05  18
03. JKT Ruvu           12  05  03  04   12   11  01  18
04. Mtibwa Sugar     10  04  05  01  13  07  06   17
05. Coastal Union    11  04  04   03  10   08  02  16
06. Polisi Moro         12  03  06  03   09  09  00  15
07. Mbeya City         11   04  03  04  08   09  -1   15
08. Ruvu Shooting    12  04  03   05   07   09  -2  15
09. Kagera Sugar     12  03  05  04   09   10   -1  14
10. Mgambo JKT      11  04  02  05   06    10  -4  14
11. Simba                11  02  07   02   11   10  01  13
12. Ndanda Fc          12  04  01   07  12    17  -5  13
13. Stand Utd           12  02  05   05   07   14  -7  11
14. Prisons               11  01  06   04   08   10  -2   09
Wafungaji:

7- Didier Kavumbagu(Azam)
6- Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)
5-Ame Ali (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Danny Mrwanda (Yanga)
4- Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba)
3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda), Nassor Kapama (Ndanda)

No comments:

Post a Comment