STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 30, 2015

Diego Simeone awakingia kifua nyota wake

http://www.fm-base.co.uk/forum/attachments/football-manager-2015-tactics/751628d1421605865-diego-simeone-4-4-1-1-simeone_1968268a.jpg
Kocha Diego Simeone
MENEJA wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeone amekataa kukosoa nidhamu ya kikosi chake baada ya mchezo wao wa Kombe la Mfalme dhidi ya Barcelona, akisisitiza anajivunia ari iliyoonyeshwa na wachezaji wake.
Atletico walimaliza mchezo huo wa robo fainali ya mkondo wa pili wakiwa wako tisa baada ya Gabi kutolewa nje kwa tukio alilofanya kipindi cha mapumziko kabla ya Mario Suarez naye kulimwa nyekundu katika dakika mwishoni na mchezo.
Naye Arda Turan pia alilimwa kadi ya njano kwa kumtupia mwamuzi wa pembeni kiatu wakati Raul Garcia yeye alipewa kadi ya njano kwa kujibizana na wajumbe walikuwa katika benchi la ufundi la Barcelona wakati wa mapumziko.
Hata hivyo, wakati akiulizwa kuhusiana na tabia za wachezaji wake baada ya kufungwa mabao 3-2 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-2, Simeone alijibu kuwa anajivunia wachezaji wake.
Simeone amesema kipindi cha kwanza kilikuwa kizuri kwani walicheza vyema na kukiri kuwa Barcelona walicheza vyema kwani wako katika kiwango cha juu toka Desemba.

No comments:

Post a Comment