STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 3, 2015

SPURS YAJIANDAA KUMTEMA ADEBAYOR

https://spursstatman.files.wordpress.com/2013/04/emmanuel-adebayor.jpgKLABU ya Tottenham Hotspurs inajipanga kumlipa Emmanuel Adebayor ili hatimaye waachane naye katika kipindi cha majira ya kiangazi. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Togo amekuwa hana namba katika kikosi cha kwanza cha Spurs, huku yeye pamoja na meneja wa timu hiyo Mauricio Pochettino wakifurahishwa na hatua hiyo pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa. 
Lakini tatizo kubwa linatarajiwa kuwa mshahara wake, kwani mshambuliaji huyo hayuko tayari kuchukua chini ya kiasi cha paundi milioni 5.2 kabla ya kuondoka. 
Hata hivyo, Spurs sasa wako tayari kulipa asilimia fulani ya mshahara wa Adebayor msimu ujao ili kuhakikisha anaondoka klabu kwao. 
Adebayor anatarajia kuingia miezi 12 ya mwisho katika mkataba wake mwishoni mwa msimu huu na anatarajiwa kuwekwa sokoni kwa mkopo au kwa dili la moja kwa moja.
Kabla ya kuchemesha mshambuliaji huyo alikuwan tegemeo White Hart Lane kwa kufunga mabao muhimu, hata hivyo kazi hiyo kwa sasa inafanywa na Harry Kane.

No comments:

Post a Comment