
Kocha Mkuu wa LIverpool, Jurgen Klopp hakuwa akimpa nafasi kubwa kama aliyokuwa nayo wakati akiichezea Aston Villa, kiasi cha Brendan Rodgers kumsajili kabla ya kutimuliwa baada ya timu kuyumba.
Kukiwa hakuna uwezekano wa kushiriki michuano ya Ulaya msimu ujao baada ya kufungwa mabao 3-1 na Sevilla katika Fainali ya michuano ya Europa League juzi Jumatano, Benteke amesema yeye sambamba na wachezaji wengine wana matumaini ya kuzungumza na Kocha Klopp kuhusu mipango ya msimu ujao. Akihojiwa Benteke amesema anafahamu kuwa bado anatakiwa kuzoea mazingira na kwasababu msimu umemalizika anadhani sasa ni wakati wa kukaa chini ya Klopp na kujaribu kutafuta suluhisho kwa ajili ya msimu ujao.
Liverpool imemaliza msimu huu wa EPL katika nafasi ya nane ikikusanya pointi 60 katika mechi 38, ikiwa ni pungufu ya pointi 21 na zile za mabingwa Leicester City.
No comments:
Post a Comment