STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 20, 2016

Kaka kashindikana Marekani kwa mkwanja mnene

http://www.trbimg.com/img-55a537e5/turbine/os-orlando-city-kaka-mls-all-star-dream-come-true-20150714
Kaka
AMA kweli wa mbili havai moja. Kiungo wa kimataifa wa Brazil, Kaka ndiye mchezaji anayelipwa zaidi katika Ligi Kuu ya Marekani-MLS, akimfunika mpaka nyota wa kimataifa wa Italia Sebastian Giovinco na nahodha wa Marekani Michael Bradley.
Kwa mujibu wa viwango vilivyotolewa jana Alhamisi, Kaka ambaye ni mshindi wa Ballon d’Or anayeichezea klabu ya Orlando City ya Florida anakunja mkwanja mnene wa Dola 7,167,500 akifuatiwa na Giovinco anayechukua Dola 7,115,556 huku Bradley yeye akichukua dola milioni 6.5.
Nyota wengine wenye majina makubwa waliojiunga na MLS katika miaka ya karibuni ndio wanafuatia akiwemo Steven Gerrard anayecheza Los Angeles Galaxy anashika nafasi ya nne kwa kupokea kiasi cha dola 6,132,500.
Nyota wa zamani wa Chelsea na Manchester City, anayeichezea New York City FC Frank Lampard anayekunja Dola Milioni 6, Andrea Pirlo Dola Milioni 5.9 na David Villa anatia kibindoni Dola Milioni 5.6.

No comments:

Post a Comment