STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 20, 2016

Kafunika! Ozil ndiye baba lao kwa Wapiga Mitutu wa Arsenal

https://d.ibtimes.co.uk/en/full/1432414/arsenal-mesut-ozil.jpg
Fundi Ozil akiwajibika uwanjani. Picha:ibtimes
KIUNGO Fundi wa kimataifa wa Ujerumani, Mesut Ozil amechaguliwa na mashabiki kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka wa klabu yaArsenal kutokana na kiwango cha juu alichoonyesha msimu huu. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 ameshinda tuzo hiyo akiwafunika Alexis Sanchez aliyeshika nafasi ya pili na Hector Bellerin aliyeshika nafasi ya tatu. 
Ozil amekuwa katika kiwango kizuri akifunga mabao nane na kutengeneza nafasi nyingine 19 msimu huu ambazo zimechagiza kwa kiasi kikubwa Arsenal kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Leicester City. Assist hizo zimemfanya Ozil kumaliza kama kinara katika Ligi Zote Tano za Ulaya na kiwango hicho pia kilimfanya Ozil kuteuliwa katika orodha ya tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa PFA ambayo ilinyakuliwa na Riyad Mahrez wa Leicester.

No comments:

Post a Comment