STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 20, 2016

Serengeti Boys yazidi kukimbiza ughaibuni


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhCvVwdCWZtJnLR9yOjg3Av_UyxK1jNNZ4RnXNg2dtnk-CEAMdOLMbnsFcZybOiAXbvZNdvXO0SonVDO_VFkVoKvzcf5BvsR-coBx_lxYzwvVA-1gxT4pbwqpR322lloUbHmyHYNr2SUJE/s640/IMG-20160402-WA0208.jpghttps://pbs.twimg.com/media/CiAFIanWMAAW1Rr.jpg 
NA TARIQ JUNIOR
TIMU ya taifa ya Vijana U17 'Serengeti Boy' imeweka mguu mmoja ndani kutinga fainali ya michuano maalum ya kimataifa ya vijana 'AIFF Youth Cup 2016' baada ya jana kutoka sare ya mabao 2-2 na Korea Kusini.
Serengeti inayonolewa na Bakar Shime imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo mwa michuano hiyo ikiwa na pointi 5 baada ya kushuka uwanjani mara tatu, huku Korea ikiwafuata nyuma yao ikiwa na pointi nne ikicheza mechi mbili tu.
Timu hiyo ya Tanzania itamaliza mechi zake keshop Jumamosi kwa kuvaana na Malaysia ili kujua hatma yake ya kucheza fainali ambayo itahusisha timu kinara na mshindi wa pili, huku zitakazoshika nafasi ya tatu na nne zitacheza mechi ya kuwania ushindi wa nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment