STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 20, 2016

Suarez bado haamini kama kamfunika Messi

http://worldsoccertalk.com/wp-content/uploads/2015/06/Suarez.jpg
Suarez
http://images.latinpost.com/data/images/full/84962/messi-neymar-suarez.jpg
Suarez, Messi na Neymar Jr wakiwa uwanjani pamoja
STRAIKA nyota wa mabingwa wa Hispania, Barcelona, Luis Suarez amesema hakutegemea kama angeweza kuchukua nafasi ya Lionel Messi ya kuwa kinara wa mashambulizi ya klabu hiyo kwa msimu huu.
Suarez amekuwa akiimarika tangu alipojiunga na Barcelona akitokea Liverpool na amefanikiwa kuibeba timu hiyo kutwaa taji la La Liga mara mbili, huku mwenyewe akimaliza kama mfungaji kinara. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay, amefunga mabao 40 katika mechi 35 za ligi alizocheza msimu huu na kumzidi mshambuliaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo katika tuzo ya Pichichi kwa kufunga hat-trick katika mchezo wao mwisho wa msimu. 
Kwasasa Messi ambaye ni mshindi wa tuzo tano za Ballon d’Or amerudi nyuma na kushambulia akitokea upande wa kushoto ili kumpisha Suarez nafasi ya katikati. 
Akihojiwa na waandishi wa habari, Suarez amesema hakutegemea kucheza nafasi hiyo kwani ndio ilikuwa ikitumiwa na Messi lakini wamekuwa wakielewana vyema ndani na nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment