STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 20, 2016

Eeh! Chelsea yamtamani tena Lukaku

http://static.standard.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2014/04/12/13/Romelu%20Lukaku.jpg
Lukaku
SIKIA hii. Klabu ya Chelsea inadaiwa kutaka kumrejesha tena mshambuliaji wao wa zamani Romelu Lukaku kutoka Everton.
Chelsea walimuuza Lukaku kwa kitita cha Pauni Milioni 28 kwenda Everton mwaka 2014, baada ya kuitumikia timu hiyo kwa mkopo na tangu wakati huo nyota huyo wa Ubelgiji, amefunga mabao 61 katika mechi 127 alizocheza. 
Chelsea iliyoshindwa kutetea taji lao la Ligi Kuu ya England (EPL) kwa msimu huu baada ya kuzidiwa ujanja na Leicester City, kwa sasa inadaiwa kutaka kumrejesha tena Lukaku, ingawa inadaiwa Everton watataka kulipwa ada ya Pauni Milioni 61 kiasi ambacho kinadaiwa kitaweza kulipwa. 
Chelsea pia inawawinda nyota wa Napoli na kinara wa mabao wa Serie A kwa msimu huu, Gonzalo Higuain na mshambuliaji wa Juventus Alvaro Morata ili kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.
Mabingwa hao wa zamani walikuwa na msimu mbovu kiasi cha kumtimua aliyekuwa Kocha wao, Jose Mourinho, lakini bado ikamaliza nafasi ya 10.

No comments:

Post a Comment