STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 3, 2016

Liverpool asikuambie mtu baba'ake imepania si utani!

http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2016/05/emre-mor-1463896209-800.jpgKLABU ya Liverpool ambayo ilikaribia kutwaa taji la UEFA Europa League kama sio kuteleza kwa Sevilla ya Hispania, imedaiwa inaongoza mbio za kuwania saini ya chipukizi wa kimataifa wa Uturuki na klabu ya Nordsjaelland, Emre Mor.
Mor mwenye umri wa miaka 18, anatajwa kama mmoja wa wachezaji bora wanaochipukia Ulaya kwasasa baada ya kuonyesha kiwango bora katika Ligi Kuu ya Denmark na kumfanya kuitwa katika kikosi cha Uturuki kwa ajili ya michuano ya Euro 2016 inayoanza Juni 10 nchini Ufaransa.
Klabu za Manchester United, Borussia Dortmund na Ajax Amsterdam nazo zinatajwa kuwa zinamwania chipukizi huyo anayemudu kiungo mshambuliaji lakini Liverpool ndio inaelezwa kuwa inaongoza mbio hizo.
Dogo huyo amefunga mabao mawili na kusaidia mengine mawili mechi 13 alizoichezea klabu yake msimu huu.

No comments:

Post a Comment