STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 3, 2016

UEFA Euro Cup 2016 itakuwa tamu si mchezo


http://www.uefa.com/MultimediaFiles/Photo/competitions/General/02/35/95/19/2359519_w2.jpg 
http://i4.irishmirror.ie/incoming/article7002411.ece/ALTERNATES/s1200/Screen-Shot-2015-12-12-at-185759.png 
http://e2.365dm.com/16/05/768x432/marcus-rashford-england_3476376.jpg?20160531141444
Rashford
http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/cristiano-ronaldo_2.jpg
Ronaldo atafanya nini safari hii huko Ufaransa

MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya Ulaya 'UEFA Euro 2016' itaanza wiki ijayo nchini Ufaransa kwa kushuhudiwa nyota wa nchi mbalimbali barani humo wakionyeshana kazi mpaka Julai 10 atakapopatikana bingwa wake.
Hispania ndio watetezi wa taji hilo ikilishikilia kwa mihula miwili mfululizo tangu mwaka 2008 na kutetea mwaka 2012.
Michuano hiyo itafanyika huku kukiwa na rekodi kadhaa ambazo zinahitajiwa kuvunjwa ikiwamo ya mchezaji alitefunga mabao mengi katika fainali moja, iliyowekwa na aliyekuwa nyota wa Ufaransa, Michel Platini mwaka 1984.
Katika michuano hiyo Platini aliyekuwa Rais wa Uefa kabla ya kufungiwa na FIFA kwa tuhuma za kifisadi, alifunga mabao 9, huku pia akitupia hat-trick mbili ikiwa ni rekodi tena zilizofululiza, mbali na bao la mapema la michuano la dakika 18.

Unajua kuwa ni nchi mbili tu za Ujerumani na Hispania ndizo zilizotwaa mara nyingi, zikifanya hivyo mara tatu kila moja, hivyo ni wakati wao wa kuzidiana ujanja au kuzubaa na kukutwa na Ufaransa inayowafukizia ikitwaa mara mbili tangu michuano ilipoasisiwa mwaka 1960.
Pia michuano hiyo ilimpa ujiko Cristiano Ronaldo mwaka 2004 alipokuwa mchezaji mwenye umri mdogo kucheza fainali akifanya hivyo mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 19 na siku 150.
Kwa kifupi kina Marcus Rashford na makinda wenzake wanapaswa kufanya mambo ili kufikia rekodi mbalimbali ambazo zimedumu kwa miaka mingi bila kuvunjwa.

No comments:

Post a Comment