STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 3, 2016

Ngeleja wenzake wapewa kifyagio na Malinzi

http://www.theworldfolio.com/img_db/timthumb.php?src=img_db/old/13226688671.jpg&w=800&z=1
Mhe. Ngeleja
http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/2841132/medRes/1098071/-/un1399/-/Jamal+Malinzi.jpg
Malinzi
MAJUZI Wabunge wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, walichagua uongozi mpya wa timu yao ya Bunge Sports Club na kama zali, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja akaukwaa Uenyekiti kilaini bila kupingwa, jambo hilo limemvutia sana Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi.
Rais huyo wa TFF amepongeza uongozi wa timu hiyo uliochaguliwa mjini Dodoma, ambapo Ngeleja alitwaa kiti akimrithi Idd Azan ambaye alishindwa kurudi bungeni katika Uchaguzi Mkuu wa Taifa wa 2015.
Mbali na Ngeleja, wengine waliopewa kifyagio hicho na Malinzi ni Makamu Mwenyekiti, Esther Matiko; Meneja wa Klabu, John Kadutu pamoja Wajumbe Neema Mgaya, Faida Bakari,  Cosato Chumi, Anna Lupembe na Grace Kihwelu.Malinzi amewatakia kila la kheri Bunge Sports Club na kuwaahidi ushirikiano kutoka TFF katika kuendeleza klabu yao na michezo kwa ujumla nchini.

No comments:

Post a Comment