STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 8, 2017

SIMBA NA YANGA HAKUNA JINSI TENA

Simba wakishangilia katika mechi zao za hivi karibuni









Picha zikionyesha kabla ya pambanio la Simba na Jang'ombe Boys lililochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Amaan.
USIYEMPENDA kaja. Simba imepata ushindi wa mabao 2-0 na kuifuata Yanga kwenye pambano la nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi katika mechi itakayopigwa usiku wa Jumanne.
Mabao mawili ya kila kipindi kutoka kwa Laudit Mavugo yametosha kuzikutanisha timu hiyo ambazo zina upinzani wa jadi katika soka la Tanzania.
Mavugo alifunga bao la kuongoza dakika ya 11 kabla ya kuongeza jingine tamu katika kipindi cha pili dakika ya 54 na kuifanya Simba kubaki kileleni mwa msimamo wa Kundi A ikiwa na pointi 10, pointi ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote nyingine iliyopo kwenye kundi hilo.
Watetezi URA ya Uganda usiku itavaana na Taifa Jang'ombe ili kuunga na Simba katika nusu fainali ambapo itakayofuzu itavaana na vinara wa Kundi B, Azam iliyoikandika usiku wa jana Yanga kwa mabao 4-0.
Katika pambano hilo lililoisha hivi punde, Simba iliwazidi ujanja wapinzani wao, licha ya Boys kujitutumua kutaka kuizuia Simba isisonge mbele.
Simba na Yanga zinakutana kwenye pambano la Kombe la Mapinduzi kwa mara ya kwanza tangu walipovaana kwenye fainali ya mwaka 2011 ambapo Yanga ilikandamizwa mabao 2-0.

Lakini hilo litakuwa pambano la nne la watani hao wa jadi kukutana visiwani Zanzibar tangu mwaka 1975 walipokutana kwa mara ya kwanza kwenye Kombe la Kagame na Yanga kushinda na kuvaana tena 1992 na Simba kushinda kwa penalti.
Washindi wa mechi za nusu fainali hizo mbili zitakazochezwa Jumanne zitavaana Ijumaa ijayo kwenye pambano la fainali ya michuano hiyo ya 11 tangu mfumo wa sasa uanze kutumika mwaka 2007 na Yanga kuwa bingwa wa awali.
Simba ndio timu iliyotwaa taji la michuano hiyo mara nyingi, ikifanya hivyo mara tatu na kufuatiwa na Azam iliyobeba mara mbili, huku Yanga, Mtibwa Sugar, Miembeni, KCCA na URA zote za Uganda zikitwaa mara moja moja.

No comments:

Post a Comment