STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 8, 2017

Mavugo atupia kambani baada ya miezi miwili

SEMENI tena! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya straika wa Simba, Laudit Mavugo kufunga bao lake la kwanza tangu alipofanya hivyo mara ya mwisho Oktoba mwaka jana katika mechi ya Ligi Kuu Bara.
Mavugo amefunga bao hilo dakika 11 ya pambano lao la Kundi A ya michuano ya Kombe la Mapinduzi unaoendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar dhidi ya Jang'ombe Boys kuwania tiketi ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo.
Kwa sasa pambano linakaribia kwenda mapumziko na Simba inaongoza bao 1-0. MICHARAZO itakuwa inakuletea dondoo kadri mechi inavyoendelea visiwani humo.

No comments:

Post a Comment