STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 8, 2017

Obi Mikel kasepa zake Uchina kiroho safi

HABARI ndio hiyo bwana! Nyota wa Chelsea John Obi Mikel ametangaza kupitia posti kwenye mitandao ya Kijamii kuwa anaihama klabu hiyo na kujiunga na klabu ya Ligi Kuu ya China, Tianjin TEDA.
Mnigeria huyo mwenye miaka 29, alijiunga na Chelsea akiwa na kinda la miaka 19 akitokea klabu ya Lyn  ya Norway mwaka 2006 na kucheza Mechi 374.
Katika msimu huu wa Ligi Kuu ya England, chini ya Kocha Antonio Conte, Mikel hajacheza hata mechi moja na inaelezwa hiyo ni sababu ya kuchukua maamuzi ya kwenda China ambayo imekuwa ikimwaga fedha lukuki kwa mastaa ili kushawishi kutua kwenye ligi yao.
Akiwa na Chelsea, Mikel alitwaa mataji 11 yakiwemo mawili ya Ligi Kuu England na moja la L:igi ya Mabingwa Ulaya.
Akiaga, Mikel alitoa shukran kwa Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich pamoja na mashabiki wa Klabu hiyo, huku bilionea huyo akimtakia kila la heri.

No comments:

Post a Comment